Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho

Mikoko: Wanawake Lamu mbioni kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa

Informações:

Sinopse

Athari za mabadiliko ya hali ya hewa hazichagui mtoto au mtu mzima, akina mama wamelichukua kuwa jukumu lao kuhakikisha mikakati imefanikishwa katika harakati za kupunguza athari hizi haswa kupitia upanzi na uhifadhi wa mikoko Katika kijiji cha Mtangawanda, jimboni Lamu pwani ya Kenya, tunakutana na kundi la akina mama ambao kupitia mafunzo, sasa ni wakereketwa wa mazingira.Licha ya changamoto mbalimbali kukiwemo dini na hata ukataji haramu wa mikoko kutokana na umuhimu wake, kinachowatia moyo ni hatua walizopiga katika kipindi cha miaka 5 iliyopita, na hata cha ziada ni kufanikiwa kuchakata tena taka za plastiki ambazo ni hatari kwa ukuaji wa mikoko.